Kit-Mikayi mwaka 2002
Kit-Mikayi (pia hutajwa kama Kit Mikayi, Kitmikayi na Kitmikaye) ni mwamba mkubwa uliyoko kwenye barabara ya Kisumu-Bondo magharibi mwa Kenya, karibu kilometa 29 magharibi mwa Kisumu. Kit-mikayi inamaanisha "Mawe ya mke wa kwanza" katika Dholuo, lugha ya Waluo.